NYOTA watano wa Simba kesho wanatarajiwa kuukosa mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya KMC unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa. Ni kipa namba tatu Ally Salim ambaye hayupo kwenye mpango wa Kocha Mkuu, Didier Gomes sawa na beki wa kushoto Gadiel Michael. Mwingine ni Jonas Mkude ambaye ana matatizo ya suala la nidhamu. Mbali na kiungo Mkude pia mshikaji wake Ibrahim Ajibu huyu yupo nje ya kikosi kwa kuwa anaumwa Malaria. Perfect Chikwende alikuwa kwenye majukumu ya timu ya taifa ya Zimbabwe

 


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii