Machapisho maarufu kutoka blogu hii
EPL UPDATES : PEP GUADIOLA KOCHA BORA EPL 2020/21
OFFICIAL - Kocha Mkuu wa Klabu ya Manchester City, Pep Guadiola, ametwaa tuzo ya kocha bora wa ligi kuu nchini England (Premier League Manager of the season) kwa msimu wa 2020-21. pep GUADIOLA ametwaa tuzo hiyo baada ya siku chache zilizopita kutwaa ubingwa wa ligi kuu England 2020/21 akiwa na Klabu ya Manchester City Tufuatilie Kwenye mitandao ya kijamii kwa @Faceboo page|Sega Sports @instagram | Sega Sports WHATSAPP +255623087983
BODI YA LIGI YAIONYA YANGA SPORTS CLUB
MTENDAJI Mkuu wa bodi ya ligi Tanzania (TPLB) Almas Kasongo ameionya Yanga kuhusu kauli ya kutopeleka timu uwanjani na kusema kwamba kanuni zinataka kuishusha madaraja mawili timu itakayofanya kitendo hicho. Kwa mujibu wa ratiba ya Ligi Kuu, mechi ya kiporo ya Simba na Yanga imepangwa kuchezwa Julai 3 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es Salaam baada ya ile ya Mei 8 kushindikana. Mechi hiyo awali ilipangwa kuchezwa Mei 8 lakini haikufanyika baada ya kutokea sintofahamu kutokana na serikali kuagizwa isogezwe mbele kutoka saa 11 jioni mpaka saa moja usiku. Msemaji wa Yanga Hassan Bumbuli juzi alinukuliwa kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii kwamba hawautambui mchezo huo kwani wao walishamaliza tangu Mei 8. Kasongo alisema jana kanuni ziko wazi kuhusu timu itayoshindwa kutokea uwanjani ikiwa ni pamoja na kushushwa madaraja mawili. “Usipopeleka timu uwanjani timu husika inashuka madaraja mawili, bado sijajua msingi wa kauli ya huyo mtu ni nini, niwakumbushe viongozi wa soka kabla hu...

Maoni